Loading...

DUUH HII INATISHA: TAZAMA KINACHOELEZWA KUWA UHUSIANO WA MTANDAO WA SHULE ZA FEZA ZILIZO KATIKA ZAIDI YA NCHI 160 NA UGAIDI NA MAPINDUZI YA UTURUKI

 

Shule za Feza zimetapakaa nchi zaidi ya 16O duniani na zinamilikiwa na mtandao unaoitwa Hizmet Movement

Hawa Hizmet Movement ni wafuasi wa Imamu wa Kituruki aishiye Marekani anyefhamika kwa jina la Fethullah Gulen
Walimu wengi wa shule hizi wametoka kwenye mtandao wa Gulen japokuwa Gulen siyo mmiliki wa shule hizo

Uhusiano wa shule hizi na uislam,

Walimu wa shule hizi wnahimiza uislamu kwenye mabweni ya shule mabapo walimu huweka mfano wa aina ya maisha anayotakiwa aishi mwanafunzi na sala
Pia zinaotoa namna ya kueneza uislamu kwa upole ili kusaidia kupunguza kuenea kwa uisilamu wa itikadi kali duniani
Hata hivyo shule hizo sio kwa ajili ya waisilamu pekee na wala haziwezi kuhesabiwa kama shule za kiislam isipokuwa kuna baadhi ya shule chache ambazo ni za Kiislam kabisa
Shule hizi zipo nchi mbalimbali duniani hasa zile zenye watu wengi wenye asili ya Uturuki kama Ujerumani, Marekani, Canada

Sifa za shule hizi
Shule hizi zimekuwa zikisifika katika nchi mbalimbali zilizopo kwa kutoa elimu bora na kuwa na kiwango kidogo cha utoro na kuhama kwa wanfunzi nchini Australia shule 17 za mtando huu zinafanya vizuri ukilinganisha na shule nyingine zianvyofanya kwenye masomo

Mtando huu wa hizi shule una agenda ya siri?
Serikali nyingi na wasomi wamekuwa wakihisi shule hizi kuwa na agenda zaidi ya kutoa elimu, Profesa wa Kituruki chuo kikuu cha Utah huko Marekani alidai shule hizi na mtandao unaozimiliki zina lengo la kisiasa, lengo hilo ni kuzalisha kikundi cha watu ambao watageuza Uturuki kuwa kituo kikuu cha dini ya Uisilamu duniani, kugeuza nchi hiyo kuwa ya kiislam na kwa sasa ndio kikundi chenye nguvu zaidi Uturuki na hakina mpinzani wa kushindana nacho

Chama kimoja cha siasa nchini Georgia kilipinga kufunguliwa kwa shule hizo Georgia kwa kuwa walikuwa na lengo la kutawalisha utamaduni wa Kituruki na dini nchini kwao na kwenye mfumo wa elimu wa nchi yao

Je kwa nini shule hizi zinahusishwa na Ugaidi?
Kumekuwa na uhimizo kutoka serikali ya Uturuki kwa nchi za Afrika kama Tanzania {walishakuja mwaka 2o13 mara ya kwanza}, Nigeria, Kenya Uganda kufunga shule hizi kwa madai ya kuwa zina jihusisha na ugaidi,

serikali nyingi zimekataa kufunga shule hizo zikidai ni mambo yao ya ndani lakini kuna baadhi ya mataifa yenye kutegemea sana Uturuki yameshazifunga, Mataifa hayo ni Somalia, Kazakhstan Uzbekistan na Tajikistan zimesha funga shule hizo tangia mwaka 2O12 kutokana na aliyekuwa wairi mkuu wa Uturuki ambaye pia sasa ndie rais Recep Tayyip Erdogan kuwataka wazifunge.
Mataifa kama Iran, Syria na Saudi Arabia hayaruhusu kabisa kufunguliwa kwa shule hizi nchini kwao

Kutakiwa kufungwa kwa shule hizi sababu sio za kigaidi bali ni za kisiasa zaidi, Yadiwa aliyepo nyuma ya mtandao huu Fetullah Gulen na rais wa sasa wa Uturuki Recep Tayyip Erdogan wana vita kutokana na mmoja kuonekana ana ushawishi zaidi Uturuki,

mahasimu hawa ambao walikuwa ni marafiki wa kisiasa wamekuja kuwa maadui baada ya skendo ya rushwa kukumba baraza la mawaziri la serikali ya Erdogan na mtoto wa Erdogan kuhusishwa

Rais huyu alitaka skendo hiyo ya rushwa isichunguzwe na wasikamatwe ili asichafue serikali yake lakini Imam Gulen alikuwa na ushawishi zaidi juu yake na mawaziri hao wakakamatwa, wakashtakiwa na kukutwa na hatia ambapo majaji na polisi hao walihisiwa ni ni wafuasi wa Gulen kutokana na kutosikiliza matakwa ya mkuu wao wa nchi

Kutokana na hili Erdogana akamtuhumu Gulen kutengeneza dola nyingine ndani ya dola ya Uturuki na kuanza kumuandama tangia mwaka 2O12, na kwenye uchaguzi wa mwaka 2O15 alipoteza majority ya wabunge wa serikali kwa kuwa alikuwa amekosana na Gulen

Gulen mwenye miaka 78 amekuwa na wafuasi wengi nchi Uturuki na amekuwa akihimiza uislamu usio na msimamo mkali na ameandika vitabu vingi kukemea ugaidi na amekuwa akionekana na kushambuliwa kama 'muisilamu mlaini' kutokana na msimamo wake huo,

Mapinduzi ya Uturuki yalikuwa ni mapinduzi feki
Baada ya kuona Gulen bado ana wafuasi wengi ndani ya nchi yake basi rais wa nchi hiyo akatafuta namna ya kuwakamata, rais huyo alipanga mapinduzi feki, kisha kuwasingizia wafuasi na askari wa Gulen ndio waliopanga mapinduzi hayo na akapata fursa ya kuwakamata, hadi sasa wamekamatwa watumishi wa umma zaidi ya 5o,ooo na amepanga kurudisha adhabu ya kifo kwa watu hao

Source:Jamii Forums
http://www.udakuspecially.com/2016/08/huu-ndio-uhusiano-wa-mtandao-wa-shule.html

Post a Comment

CodeNirvana
Newer Posts Older Posts
© Copyright Amour | Designed By AFROPIXELS MEDIA CO. LTD
Back To Top